Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

ISO 9001:2015 Imethibitishwa Kutoa Huduma za Hali ya Hewa kwenye Usafiri wa Anga

10 Days Forecast

MUHTASARI WA MWENENDO WA MVUA KWA TAREHE 01-10 FEBRUARI, 2026 NA MATARAJIO YA MVUA KWA TAREHE 11-20 FEBRUARI, 2026

MWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 11-20 FEBRUARI, 2026.

Kanda ya ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika maeneo machache.

Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Vipindi vya Mvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache.

Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam      pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba):  Vipindi vya Mvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache.

Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo.

Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Vipindi vya mvua zinazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.

Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo.

Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika maeneo machache.

Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo.

Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua...