Taarifa za Utabiri
Upepo wa Pwani: Unatarajiwa kuvuma kutoka Mashariki kwa kasi ya km 20 kwa saa kwa Pwani ya Kusini na kutoka Kusini Mashariki kwa kasi ya km 30 kwa saa kwa Pwani ya Kaskazini. Hali ya Bahari: Inatarajiwa kuwa na Mawimbi madogo hadi Makubwa Kiasi.
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua....
MWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 11-20 0KTOBA, 2025
Kanda ya ziwa Viktoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Vipindi vya mvua zinazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Hali ya ukavu kwa ujumla inatarajiwa.
Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaampamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache.
Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Hali ya ukavu kwa ujumla inatarajiwa.
Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Hali ya ukavu inatarajiwa.
Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Hali ya ukavu inatarajiwa.
Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Vipindi vya mvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Hali ya ukavu kwa ujumla inatarajiwa.
Imetolewa na:
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Kwamaelezo zaidi tafadhali pakua...
- Dondoo za tathmini ya Septemba, 2025 na mwelekeo wa Oktoba, 2025:Taarifa hii inatoa muhtasari wa mifumo ya hali ya hewa pamoja na mwenendo wa hali ya hewa kwa mwezi Septemba, 2025 na kutoa mwelekeo wa hali ya hewa kwa mwezi Oktoba, 2025 nchini. i.Katika kipindi cha mwezi Septemba, 2025 hali ya ukavu pamoja na vipindi vya baridi hususan katika nyakati za usiku vilijitokeza katika maeneo machache. Hata hivyo, vipindi vichache vya mvua vilijitokeza katika baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani, nyanda za juu kaskazini mashariki na ukanda wa ziwa Victoria.ii.Katika kipindi cha mwezi Oktoba 2025, mvua za Vuli zinatarajiwa kuanza katika maeneo mengi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. Aidha, mvua za chini ya wastani hadi wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi.iii.Katika kipindi cha Oktoba, 2025, ongezeko kidogo la joto linatarajiwa katika baadhi ya maeneo.
Kwa maelezo zaidi, tafadhali pakua
Dondoo muhimu za mvua za Msimu (Novemba, 2025 – Aprili, 2026)
Taarifa hii inatoa uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka (kanda ya magharibi, kati, nyanda za juu kusini magharibi, kusini mwa nchi, ukanda wa pwani ya kusini pamoja na maeneo yaliyopo kusini mwa Mkoa wa Morogoro) katika kipindi cha miezi ya Novemba, 2025 hadi Aprili, 2026. Ushauri na tahadhari umetolewa kwa wadau wa sekta mbalimbali wanaotumia taarifa za hali ya hewa katika utekelezaji wa majukumu yao kama vile kilimo na usalama wa chakula, mifugo na uvuvi, maliasili, wanyamapori na utalii, nishati na maji, ujenzi, usafiri na usafirishaji (nchi kavu, kwenye maji na angani), mamlaka za miji, afya, sekta binafsi pamoja na menejimenti za maafa. Muhtasari wa mwelekeo wa mvua hizo na athari zake ni kama ifuatavyo:
a) Mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka:
(i) Mvua za Chini ya Wastani hadi Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Singida na Dodoma. Aidha, mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa, Ruvuma, Mtwara na Lindi pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro. Msimu unatarajiwa kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha katika maeneo mengi.
(ii) Mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba, 2025 katika mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma; na kusambaa katika mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro kati ya wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Novemba, 2025. Mvua hizi zinatarajiwa kuisha kati ya wiki ya nne ya mwezi Aprili na wiki ya kwanza ya mwezi Mei 2026 katika maeneo mengi.
(iii) Kipindi cha nusu ya pili ya msimu (Februari – Aprili, 2026) kinatarajiwa kuwa na ongezeko la mvua ikilinganishwa na nusu ya kwanza (Novemba, 2025 – Januari, 2026).
b) Athari na ushauri
(i) Mvua za Chini ya Wastani zinazotarajiwa katika maeneo mengi zinaweza zikasababisha upungufu wa unyevu wa udongo, jambo ambalo linaweza kuathiri ukuaji na maendeleo ya mazao na kupunguza mavuno hususani kwa mazao yanayategemea mvua.
(ii) Kupungua kwa kina cha maji kwenye mabwawa na mtiririko wa maji kwenye mito kunaweza kutokea, hali ambayo inaweza kupunguza upatikanaji wa maji kwa matumizi mbalimbali.
(iii) Upatikanaji wa maji na malisho kwa ajili ya mifugo unatarajiwa kuathirika.
Kwa maelezo zaidi rafadhali pakua.
Dar es Salaam |
|||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|
Tarehe | Hali ya Mchana | Kiwango cha Juu cha Joto | Kiwango cha Chini cha Joto | Mawio ya Jua | Machweo ya Jua | ||
19/10/2025 |
![]() Vipindi vya Jua |
31°C | 21°C | 06:05 | 18:15 | ||
19/10/2025 |
![]() Mvua Nyepesi |
30°C | 21°C | 06:05 | 18:15 | ||
20/10/2025 |
![]() Vipindi vya Jua |
31°C | 21°C | 06:05 | 18:15 | ||
19/10/2025 |
![]() Mvua Nyepesi |
30°C | 21°C | 06:05 | 18:15 | ||
20/10/2025 |
![]() Vipindi vya Jua |
31°C | 21°C | 06:05 | 18:15 |