Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania
ISO 9001:2015 Certified in Aviation Meteorological Services
WATAALAMU WA HALI YA HEWA KUHAKIKISHA USAHIHI WA UTABIRI WA MVUA ZA MASIKA UNAKUWA WA HALI YA JUU
Imewekwa: 11th February, 2019
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania
(TMA) Dkt. Agnes Kijazi amewata wataalam wa hali ya hewa kutumia utalaam
wao walionao kuhakikisha maandalizi ya utabiri wa hali ya hewa kwa
msimu wa mvua za masika (Machi hadi Mei2019) unaendelea kuwa sahihi
zaidi katika kiwango cha juu na wenye ubora utakaosaidia maendeleo ya
kiuchumi katika taifa letu. Dkt. Kijazi alizungumza hayo wakati wa
kufungua warsha ya wataalamu wa hali ya hewa katika kuandaa utabiri
huo. Warsha hiyo itafuatiwa na warsha ya
wataalamu mabingwa wote wa hali ya hewa pamoja warsha ya wadau wa huduma
za hali ya hewa na warsha ya wanahabari kabla ya kutoa rasmi mwelekeo
wa msimu wa mvua za MASIKA 2019 tarehe 14 Februari 2019.
© 2019 Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania. Haki zote zimehifadhiwa.